CURRENCY CONVERTER

FreeCurrencyRates.com

New Ads

Educationmakala mbalimbalisimulizi

FUATILIA PIA STORY NZURI NA YA KUSISIMUA IITWAYO "BARUA KWA MAMA"

SuraYa  1

Ni miaka mitano sasa tangu nilipojikuta nikiwa katika nazingira haya yaliyogubikwa Kwa wingiwa shida, karaha na kila aina ya uzuni. Nyumbani kwetu napakumbuka japo nilitoka tangu kitambo baada ya maisha ya kutafuta Nile nini, nitasomaje Na nitakuwa Na picha gani katika jamii hii ambayo humthamini binadamu kwa kuangalia hadhi yake katika kipato yaani maisha mazuri ya kuweza kutatua maisha yake ya wenye shida, na elimu aliyonayo mtu ndiyo alama ya kumfanya mtu aonekane wa thamani katika jamii. Jamii iliyojaza watu wa aina mbalimbali na wenye tabia, huruka, mwenendo na maono mbalimbali ni jamii inayofaa kwa mwanasayansi au mtafiti yeyote kuzisoma jamii zote duniani kuwa ni nini hasa kinazikumba familia na jamii nyingi kwa ujumla.
Kwa aliye wakwanza kusimulia ndiye wa kwanza kuona, au pengine imemgusa kuwa wa kwanza ama kutangulia kusema. Mbona unaongea kwa mafumbo makali ambayo yananipa shida kuyafumbua? Aliuliza Boraman! Rafiki yangu kadili ninavyoendelea Kunene maneno haya ambayo ama hakika yamezungukwa na kuroanishwa kwa machozi ya uzuni mwingi kwani kwa haya ninayoyaona na ninayoyasikia yananifanya nifahamu kuwa watu wengi katika jamii huishi kwa mashindano na kutamani wawebora kuliko viumbe vingine hapa katika ulimwengu wa Musa. Unadai huelewi kwa fumbo hili dogo yaani kama lingekuwa yai la mchemsho hata kibogoyo angetafuna na wewe ungebaki kumeza mate na uso kuliokunjika kama safu za milima mikunjo. Mifano ndiyo njia yaw ewe kunielewa.
Hapo zamani kulikuwepo na mfalme katika kijiji cha Hira, ambacho kilitawaliwa kwa nguvu za miungu na uchawi. Siku moja mfalme wa Hira aliitisha kikao cha dharura ambacho hukaliwa mara moja kwa mwaka hasa katika kusherekea sherehe za mavuno au majadiliano kuhusu majanga yaliyokikumba kijiji hicho ambayo huwa ni mafuriko yanayosababisha mavuno hafifu, ukame unaopelekea kukauka kwa mazao, na tetemeko la aridhi ambalo huwashitua watu hasa nyakati za usiku napengine mchana wakati wa shughuli za kilimo au mavuno zikiendelea.
Haijawahi kutokea mfalmekwa Hira kuwaita wanakijiji wa mambo mawili au Zaidi bali huwaita kwa jambo mojamoja ili apate kujadili kwa kina na watu wake. Siku moja hakukuwa na tukio lolote la kufanya watu waitwe ili kuelezwa jambo kwani ilikuwa ni yapata mwezi wa sita, wiki ya sita, siku ya sita ya wiki, saa sita mchana na dakika sita ndipo Mfalme aliwatuma walinzi wake wakazunguke kijijini kote kuwapasha habari watu kuwa kesho ni siku ya saba saa saba mchana na dakika saba ndio muda wa kila mmoja pale kijijini kuwa amefika kwa Mfalme ili kusikia alichokiandaa kukisema.
Gafla sauti ikasikika kutoka katika pembe  nne za nyumba ya Mfalme iliwa na ujumbe wa maneno manne yaliyosemwa baada ya dakika nne kupita kwamba HATUTAKI UFANYE KAMA UNAVYOTAKA Mfalme alisikiliza kwa makini lakini kutekeleza agizo alikuwa tayari ni mchelewaji. Alilia kwa maamzi yake kuwakimbilia walinzi kuwakataza ilikuwa tayari maji yamezidi unga kwani walikuwa wameisha kutana na vijana watano waliokuwa wameongozana na mbwa watano na mabega yao hadi mgongoni ipo michilizi ya damu za wanyama waliowabeba mabegani waliwambia kuwa, kesho saa saba na dakika saba ndio muda wa kuanza kikao na Mfalme wa Hira ili aseme aliyonayo na nyie muliopata taarifa hizi basi kumbuka kuwambia na wenzenu mtakaofanikiwa kuonana nao katika sehemu zenu za mapumziko.
Mfalme alipiga moyo konde na kusema sawa! Lakini siamini kuwa kusema adhima yangu ni vibaya. Lakini mizimu yangu nipo chini ya unyayo wenu, nifanye mteule na mkuu kuliko wote hapa kijijini kwani nimetawala miaka mingi na kwa unyenyekevu mkubwa sana kwa nilipofikia nahitaji kuwa tofauti na watu wa kawaida. Sauti yao ikasikika tena kwa mara nyingine ikisema kuwa japo wataka uonekane wa tofauti na wengine je? unataka miguu mitatu, mikono mitatu au uso wa mbele na nyuma? Alitetemeka sana huku akiwa katika majonzi ya kwanini kaamua kufanya vile bila kuuliza lakini Mfalme alijipa moyo kwa kusema kosa siyo kosa bali kosa ni kurudia kosa. Nitaendelea ili kutimiza hili japo nyie hampendi lakini musinihaibishe mbele ya wananchi wangu, kwani natambua sitakiwi kuendana kinyume na ninyi wakuu wangu mliyenipa rungu hili la kukiongoza kijiji hiki yapata miaka sabini tangu nikiongoza nikiwa na miaka saba.
Akiwa anajibizana na mizimu ya kuzimu, gafla waliludi walinzi na kukaa chini pia kunyoosha miguu mbele na mikono kuilaza mapajani kisha mmoja wao wawili akasema kwa sauti ya kusikika vizuri MTUKUFU MFALME!! Mfalme alishituka sana na kujikuta kamukanyaga, Kahiramulinzialiyeagizwa na Mfalme kuwa waambatane kusambaza habari hizo, Kahira hakuwa na shaka la kukatisha maneno yake japo kama ilivyo kwa binadamu alishituka lakini baadae akaendelea japo alirudia kusema mtukufu mfalme kazi uliyonituma nimeifanya kadili ya unavyotaka na kufika kesho saa saba kamaili katika sekunde ya saba watu watakuwa wamejaa hapa kama kwenye soko la mitumba hasa karibia sherehe za krismas. Mfalme alijibu kuwa kama umefanya kama nilivyokutuma asante sana japo ni jukumu lako. Pia Kahira alisema pia mtukufu mfalme, kwa bahati mbaya zaidi nimejikuta nimeweka mguu wangu chini ya mguu wako huo wa kushoto. hivyo, nisamehe sana mtukufu mfalme kama itakupendeza naomba nitoe mguu wangu. Mfalme alicheka sana na kuendelea kuamini kuwa yeye ni kila kitu na anahitaji kilichobaki kimoja ili awe juu Zaidi.
Kufikia saa saba siku iliyofuata watu walimiminika kama kwa wingi na haraka sana kama risasi zinazopigwa mfululizo, Mfalme alisimama mbele yao haya hakusubili akalibishe na mlinzi wake bali aliwataka wananchi wa Hira kwa kusema samahani wananchi leo kama kawaida yetu siyo siku maalumu kwa kukutana ilia nimewahitaji huku nikitambua fika kuwa hapa kijijini tunavyovipawa vingi kwani mfalme ninashida inayotakiwa itatuliwe na mmoja wenu hapa.
Mimi nimekuwa mtawala wa kijiji hiki yapata miaka sabini sasa hivyo nimelidhika na kuwa mfalme japo nitabaki kuwa mfalme lakini na hitaji mganga mmoja ambaye atanitengenezea pete ambayo nikienda harusini baada ya muda nikiitazama nifurahi huliko yeyote pale hata bwana harusi pia nikienda msibani nikiitazama nihuzunike kuliko wote hata kumzidi yule baba mgane aliyeondokewa na mke wake kipenzi.

No comments:

Post a Comment

Bottom Ad [Post Page]